Mvua, radi sababu mchezo wa Ufaransa, Iraq kusimama
Muktasari:
- Kabla ya kumalizika kwa dakika 45 za kipindi cha kwanza, mvua kubwa ilianza kunyesha hadi wakati wachezaji wanaenda vyumbani kwa ajili ya mapumziko, bado ilikuwa inaendelea ikiambatana na radi.
Mchezo wa Kombe la Dunia kati ya Ufaransa na Iraq umesimamishwa kwa muda kutokana na mvua kubwa iliyonyesha katika Uwanja wa Lincon Finacial Field, Marekani
Mvua hiyo ilianza kunyesha zikiwa zimebaki dakika chache kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza cha mchezo huo, huku ikiambatana na radi.
Baada ya dakika 45 za kipindi cha kwanza kumalizika, wachezaji waliingia vyumbani huku mvua ikiendelea kunyesha. Hata baada ya mapumziko ya dakika 15, hali ya hewa haikuruhusu mchezo kuendelea na wachezaji kushindwa kurejea uwanjani.
Mchezo huo umeenda mapumziko Ufaransa akiaa kifua mbele kwa bao 1-0 likifungwa na Kylian Mbappe.
Endelea kufuatilia Mwanaspoti kwa taarifa zaidi.