Madueke mawazo yote yapo Emirates
Muktasari:
- Kocha wa Chelsea, Enzo Maresca alisema winga huyo amechukua uamuzi wa kwenda kujiunga na wapinzani wao wa London kwa ajili ya mikikimikiki ya Ligi Kuu England msimu ujao.
LONDON, ENGLAND: WINGA wa Chelsea, Noni Madueke hakujali kuhusu fainali ya Kombe la Dunia la Klabu inayopigwa Jumapili baada ya kuondoka kwenye kambi ya timu hiyo kurudi London kwenda kuanza maisha mapya kwenye kikos cha Arsenal.
Kocha wa Chelsea, Enzo Maresca alisema winga huyo amechukua uamuzi wa kwenda kujiunga na wapinzani wao wa London kwa ajili ya mikikimikiki ya Ligi Kuu England msimu ujao.
Madueke, 23, amekubali mkataba wa miaka mitano ya kujiunga na Arsenal katika dili litakalogharimu Pauni 52 milioni.
Kocha Maresca alisema: “Noni yupo kwenye mawasiliano na klabu mpya na nadhani atakwenda huko. Nilishawahi kusema, kama wachezaji wanataka kuondoka, hilo litakuwa jambo gumu kwa klabu na kocha. Noni ameamua kuondoka, hakuna aliyemwambia Noni aondoke. Kama anafuraha, tunafurahi.”
Maresca hivi karibuni alisifu kiwango cha Madueke kwenye fainali za Kombe la Dunia la Klabu na hakuwa tayari kuachana na Mwingereza huyo aondoke.
Lakini, ujio wa winga Jamie Gittens, pamoja na mastraika Liam Delap na Joao Pedro, hiyo ina maana, Chelsea itahitaji kuuza baadhi ya wachezaji ili kuweka sawa vitabu vyao vya mishahara.
Chelsea itaingia uwanjani kukipiga na Paris Saint-Germain kwenye fainali ya Kombe la Dunia la Klabu na kocha Maresca alisema watakwenda kupambana bila woga.
Alisema: “Nani kasema? Tutakwenda kujuana hukohuko. Sawa wenzatu ni timu yenye kiwango cha juu, timu bora duniani. Lakini, kila mechi ni tofauti. Tutakwenda kuonyesha ubora wetu.”
MADUEKE vs MAWINGA
WENGINE WA ARSENAL
-Mechi: Trossard 38, Martinelli 33, Madueke 32
-Mabao: Trossard 8, Martinelli 8, Madueke 7
-Asisti: Trossard 7, Martinelli 4, Madueke 3
-Tachi kwa dk90: Trossard 50, Martinelli 42, Madueke 47
-Pasi kwa dk90: Trossard 30, Martinelli 23, Madueke 26