Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Heskey ataja wa kumrithi Mo Salah

Muktasari:

  • Mo Salah alisaini mkataba wa miaka miwili kusalia Anfield majira ya joto yaliyopita, lakini sasa yuko katika miaka yake ya 30 na msimu huu umeonyesha dalili za kwanza za kushuka kwa kiwango. Kauli yake ya hasira katikati ya msimu iliongeza tetesi kwamba huu unaweza kuwa msimu wake wa mwisho katika kikosi hicho cha Anfield.

LIVERPOOL, ENGLAND: NYOTA wa zamani wa Liverpool, Emile Heskey, ametaja wachezaji anaowaona wanaweza kuchukua nafasi ya Mohamed Salah na kusema kuwa nyota wa Paris Saint-Germain, Khvicha Kvaratskhelia, “ndiye chaguo langu la kwanza”.

Mo Salah alisaini mkataba wa miaka miwili kusalia Anfield majira ya joto yaliyopita, lakini sasa yuko katika miaka yake ya 30 na msimu huu umeonyesha dalili za kwanza za kushuka kwa kiwango. Kauli yake ya hasira katikati ya msimu iliongeza tetesi kwamba huu unaweza kuwa msimu wake wa mwisho katika kikosi hicho cha Anfield.

Salah amekuwa na rekodi ya mabao ya ajabu akiwa Liverpool na sasa anahesabiwa miongoni mwa wachezaji bora zaidi kuwahi kuichezea klabu hiyo. Hata hivyo, klabu italazimika kutafuta mbadala wake mapema au baadaye. Mchango wake msimu huu umekuwa wa kawaida ukilinganisha na misimu iliyopita, lakini bado ataacha pengo kubwa sana.

Kvaratskhelia amefanya vizuri sana jijini Paris, akiisaidia timu kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya  msimu uliopita, licha ya kuhamia kutoka Napoli katikati ya msimu zaidi ya mwaka mmoja uliopita. Heskey anaona kuwa ndiye mbadala bora, huku nyota wa West Ham United, Jarrod Bowen, pia akiwa kwenye orodha yake ya matamanio.

Heskey aliiambia OLBG: “Tunazungumzia kumrithi Mohamed Salah na kama mashabiki lazima uangalie kitu tofauti kwa sababu huwezi kumrithi Mo Salah moja kwa moja. Nakumbuka msimu mmoja mtu aliniambia Mo amekuwa na msimu mbaya, alikuwa amefunga mabao 25. Ningependa kuwa na ‘msimu mbaya’ kama huo. Tunazungumzia mchezaji anayefunga mabao zaidi ya 20, karibu 30 kila msimu kwa miaka 10.

“Sidhani kama unaweza kumrithi Mo Salah moja kwa moja, lakini nampenda yule kijana wa PSG, Khvicha Kvaratskhelia. Ndiye ningemchagua kwanza. Je, Jarrod Bowen atakuwa chini ya kiwango cha Mohamed Salah? Nafikiri wachezaji wengi watakuwa chini ya kiwango chake, lakini ukweli ni kwamba Bowen ni aina tofauti ya mchezaji na anaweza kusaidia mfumo kwa sababu atafanya kazi kwa bidii zaidi kidogo kuliko Mo.”

Heskey pia amemtaja Christian Pulisic kama lengo linalowezekana, licha ya kushindwa kuwa na kiwango thabiti akiwa Chelsea. Alikuwa na vipindi vizuri, lakini klabu hiyo iliridhia kumuuza na sasa anacheza katika kikosi cha AC Milan.