Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

BURGER ZILIMPONZA ANDERSON

LONDON, ENGLAND. NYOTA wa zamani wa  Manchester United,  Rafael anaamini kwamba aliyekuwa mchezaji mwenzake wa mashetani wekundu wa Old Trafford, Anderson angekuwa bora Dunia  lakini aliponzwa na tabia yake ya kupenda kula hovyo  burger.

Anderson  alijiunga na Manchester United. 2007 akitokea FC Porto ya Ureno  akiwa mmoja kati ya  wachezaji ambao walikuwa wakionekana kuwa anaweza  kufanya makubwa.

Kiungo huyo alijikuta akicheza fainali moja tu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, 2008 akiwa na Manchester United dhidi ya Chelsea kabla ya taratibu kuanza kuongezeka uzito.

Rafael, ambaye kwa sasa anaichezea  Istanbul Basaksehir alisema, "Tatizo ni kwamba alikuwa akiumia mara kwa mara na kingine chakula ambacho alikuwa akipenda kula, kiwango chake kiliathirika."

Aliendelea kumuongelea Mbrazil mwenzake kwa kusema, "Alikuwa akionyesha kiwango kikubwa sana akiwa kwenye ubora wake, nadhani angekuwa mmoja wa wachezaji bora kabisa Duniani."

Licha ya kwamba Anderson alikipiga Old Trafford kwa miaka saba na miezi kadhaa, aliondoka jijini Manchester  akiwa mchezaji wa kawaida tofauti na vile ambavyo alikuwa akitazamiwa na kujikuta akirejea nyumbani kwao, Brazil kwa kujiunga na Internacional.