Bundesliga, Ligue 1, Serie A kutamu
Muktasari:
- Kwenye Bundesliga, FC Heidenheim itakipiga na Borussia Monchengladbach, wakati RB Leipzig itacheza na Mainz 05, St. Pauli na Borussia Dortmund, VfL Bochum na Hoffenheim, Werder Bremen na Wolfsburg na Eintracht Frankfurt itamaliza ubishi na Bayer Leverkusen, huku Union Berlin ikicheza na Holstein Kiel na Augsburg itakuwa na kibarua kizito mbele ya Freiburg.
MUNICH, UJERUMANI: KIVUMBI leo. Ndicho unachoweza kusema kutokana na kile kinachokwenda kutokea kwenye mikikimikiki ya Ligi Kuu za Ulaya, hasa Bundesliga, Ligue 1 na Serie A. Ni moto.
Kwenye Bundesliga, FC Heidenheim itakipiga na Borussia Monchengladbach, wakati RB Leipzig itacheza na Mainz 05, St. Pauli na Borussia Dortmund, VfL Bochum na Hoffenheim, Werder Bremen na Wolfsburg na Eintracht Frankfurt itamaliza ubishi na Bayer Leverkusen, huku Union Berlin ikicheza na Holstein Kiel na Augsburg itakuwa na kibarua kizito mbele ya Freiburg.
Huko kwenye Ligue 1, macho ya wengi yatakuwa kwenye kivumbi cha PSG na Lille, lakini Saint-Etienne itakuwa na kazi kwa Nice, huku Lens itacheza na Le Havre, Lyon na Brest, Angers na Toulouse, Auxerre na Strasbourg, Montpellier na Rennes na vigogo Marseille watakuwa nyumbani kutoana jasho na Nantes.
Vumbi la Italia kwenye Serie A, mambo yataanza na Atalanta ikikipiga na Venezia, wakati kasheshe la wikiendi litakuwa baina ya Napoli na Inter, wakati Udinese itaonyeshana ubabe na Parma, Monza na Torino, Bologna na Cagliari, Genoa na Empoli, huku AS Roma itakuwa na kibarua kizito mbele ya chama la Cesc Fabregas, Como 1907 na vigogo wa soka la Italia, AC Milan watajitupa San Siro kukamuana na Lazio.