Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Benzema atetewa EURO 2020

BARCELONA, HISPANIA. KARIM Benzema, 33, alirudishwa kwa mbwembwe kwenye timu ya taifa ya Ufaransa ili kuisaidia katika Kundi la Kifo la Euro 2020 baada ya kutengwa na kocha Didier Deschamps kwa miaka sita. Lakini tangu amerejea hajafanya kilichotarajiwa na staa wa timu hiyo, Antoine Griezmann, amejitokea kumkingia kifua.

“Benzema akifunga bao moja tu mengine yatakuja,” alisema Griezmann kuhusu staa huyo ambaye alikuwa na kiwango bora kabisa Real Madrid, ambako alifunga mabao 30 katika mechi 46.