Anthony Gordon apewa miaka mitano Barcelona
Muktasari:
- Winga huyo wa England awali alitarajiwa kutambulishwa mapema zaidi siku hiyo, lakini hafla ya utambulisho ilicheleweshwa kwa muda kutokana na taratibu za mwisho za kodi na masuala ya kiutawala yaliyohusiana na nyaraka za uhamisho.
FC Barcelona wametangaza rasmi usajili wa Anthony Gordon baada ya kukamilisha hatua za mwisho za uhamisho wake leo Ijumaa Mei 29,2026.
Winga huyo wa England awali alitarajiwa kutambulishwa mapema zaidi siku hiyo, lakini hafla ya utambulisho ilicheleweshwa kwa muda kutokana na taratibu za mwisho za kodi na masuala ya kiutawala yaliyohusiana na nyaraka za uhamisho.
Licha ya kuchelewa huko, Barcelona walithibitisha kuwa hakukuwa na tatizo lolote kwenye makubaliano hayo na kusisitiza kuwa dili hilo lilikuwa linaendelea kama ilivyopangwa.
Maafisa wa klabu walieleza kuwa nyaraka zote zilizobaki zilikamilishwa kwa mafanikio kabla Gordon hajasaini rasmi mkataba wake katika ofisi za Commercial Office za klabu. Baadaye, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 alipiga picha akiwa amevaa jezi ya Barcelona na anatarajiwa kuzungumza na waandishi wa habari katika hafla yake rasmi ya utambulisho.
Gordon anaijiunga na Barcelona baada ya kuwa na kipindi kizuri katika Newcastle United, ambapo kiwango chake kilivutia vilabu vikubwa kadhaa vya Ulaya, ikiwemo Liverpool FC na FC Bayern Munich.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa England anaonekana kuwa nyongeza muhimu kwa kocha wa Barcelona Hansi Flick pamoja na mkurugenzi wa michezo Deco, ambao wote walikuwa wakisisitiza kuimarisha safu ya ushambuliaji ya klabu hiyo kabla ya msimu mpya kuanza.
Baada ya kukamilisha shughuli zake za utambulisho, Gordon anatarajiwa kujiunga na timu ya taifa ya England huku maandalizi ya FIFA World Cup ya majira haya ya kiangazi yakiendelea.