Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Yanga yaisulubu Polisi Zanzibar kombe la Mapinduzi

Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia moja ya mabao yao walipocheza na timu ya Polisi ya Zanzibar kwenye Kombe la Mapinduzi. Yanga ilishinda 4-0

Muktasari:

Ushindi huo ni wa pili mfululizo kwa Yanga ambayo katika mechi yake ya kwanza Ijumaa iliyopita iliifunga Taifa Jang’ombe mabao 4-0 na sasa inaongoza Kundi A ikiwa na pointi sita na mabao manane, haijafungwa hata bao moja.

HATUREMBI! Hii ndiyo kauli ya Yanga jana Jumapili baada ya kuendeleza ushindi katika michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kuifunga Polisi Zanzibar mabao 4-0 kwenye Uwanja wa Amaan.

Ushindi huo ni wa pili mfululizo kwa Yanga ambayo katika mechi yake ya kwanza Ijumaa iliyopita iliifunga Taifa Jang’ombe mabao 4-0 na sasa inaongoza Kundi A ikiwa na pointi sita na mabao manane, haijafungwa hata bao moja.

Katika mchezo wa jana, Polisi ilionekana kucheza vizuri dakika 20 za kwanza lakini haikuweza kuhimili kasi ya Yanga na kujikuta ikiruhusu bao dakika ya 27 lililofungwa na Andrey Coutinho raia wa Brazil. Coutinho alifunga bao hilo baada ya kuuwahi mpira uliorushwa na beki Oscar Joshua.

Straika wa Yanga, raia wa Liberia Kpah Sherman aliifungia timu yake bao la pili dakika ya 33 akimalizia pasi safi ya kichwa ya Amissi Tambwe.

Bao hilo liloonekana kuwa jepesi baada ya kipa wa Polisi, Omar Mzee kushindwa kuokoa shuti hilo hafifu la Sherman. Mabao hayo yalidumu hadi mapumziko.

Kipindi cha pili Yanga iliendeleza kasi yake na kufanikiwa kupata bao la tatu kwa mpira wa adhabu uliopigwa na Coutinho dakika ya 56 baada ya straika Mrundi Amissi Tambwe kuangushwa nje kidogo ya eneo la hatari.

Kwenye mchezo huo Coutinho alikuwa mwiba kwa mabeki wa Polisi ambao kila mara aliwazidi ujanja.

Licha ya Polisi kujitahidi kucheza kwa uangalifu na kutumia nguvu, Yanga iliendelea na kasi yake na winga Simon Msuva aliipatia bao la nne dakika ya 80 akimalizia pasi ya kiungo Salum Telela.

Bao hilo limemfanya Msuva kufunga mabao manne katika michuano hiyo baada ya kufunga mabao matatu ‘hat trick’ katika mchezo dhidi ya Taifa Jang’ombe.

Kocha wa Yanga, Hans Van Der Pluijm alisema: “Nafurahi tumeshinda mabao mengi lakini bado sijaridhika na kiwango cha washambuliaji, wanapoteza nafasi nyingi jambo ambalo linaweza kutugharimu huko baadaye”

Kwa upande wake, Kocha wa Polisi, Hamis Sufiani, alisema: “Nasikitika kwa matokeo haya, mipango yetu yote imefeli lakini tutapambana mechi ya mwisho kuhakikisha tunasonga mbele.”

Yanga; Ally Mustapha ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Cannavaro/Rajab Zahir, Kelvin Yondani, Salum Telela, Simon Msuva, Nizar Khalfan/Hassan Dilunga, Amissi Tambwe, Kpah Sherman/Danny Mrwanda, Andrey Coutinho/Mrisho Ngassa.

Polisi; Omar Mzee, Mohamed Seif, Mwita Makame, Mohamed Chaibu, Abdallah Kheri, Ally Khalid, Mohamed Vuai, Said Bakari, Frank Ikobela, Samir Mushekhe na Daniel Joram.

Katika mechi ya awali, KCCA ya Uganda ambao ndio mabingwa watetezi waliibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mtende FC. Wafungaji wa mabao hayo ni Herman Waswa dakika ya 41, William Wadri aliyefunga mawili dakika ya 65 na 66.

Katika mechi ya Ligi Kuu Bara jana Jumapili, Ndanda Fc ya Mtwara iliifunga Prisons ya Mbeya bao 1-0 na kupanda hadi nafasi ya 12 kwenye msimamo wa ligi na pointi zake tisa.