Yanga pesa yenu tu kwa Luhende

Muktasari:
Luhende aliyebakiza miezi michache kumaliza mkataba wake wa mwaka mmoja na Mtibwa, amesema wala hana tatizo na Yanga, pesa yao tu.
YANGA ipo katika mkakati wa kuhakikisha inamrudisha kundini beki wa kushoto, David Luhende, kutoka Mtibwa Sugar.
Luhende aliyebakiza miezi michache kumaliza mkataba wake wa mwaka mmoja na Mtibwa, amesema wala hana tatizo na Yanga, pesa yao tu.
Luhende aliondoka Yanga kabla ya kuanza kwa msimu huu baada ya uongozi kushindwa kumpa mkataba mpya, kikosini Mtibwa amekuwa akifanya vizuri na kupitia mmoja wa viongozi wake, Yanga imeanza mipango ya chinichini kuhakikisha Luhende anarudishwa kikosini ili kusaidiana na Oscar Joshua.
Juu ya hilo, Luhende amesema: “Naelekea kumaliza mkataba wangu Mtibwa, si Yanga tu, timu yoyote ije tuzungumze cha kufanya, mpira ndio kazi yangu.”