Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Yanga kushusha kifaa Afrika Kusini

Rais wa Yanga, Hersi Said amesema wanafuatilia kama mchezaji nyota wa Kaizer Chiefs, Khama Billiat (32) ataongeza mkataba klabuni hapo kwakuwa ni miongoni mwa wachezaji walio kwenye rada yao.

Billiat ambaye ni raia wa Zimbabwe mkataba wake unafikia mwisho msimu huu, amekuwa nje ya uwanja mzunguko wa pili Ligi Kuu nchini humo kutokana na majeraha lakini tayari ameshaanza mazoezi na haijajulikana kama ataweza kucheza mechi ya mwisho ya msimu.

Akihojiwa na kituo cha FARPost, Hersi amesema; "Ukiniuliza mimi ni moja ya wachezaji ninaowakubali, ubora wake ni mkubwa sana. Kwahiyo kwanini kama tukipata nafasi ya kuwa nae?

Makamu wa Rais wa timu hiyo, Arafat Haji pia amesema watajadili kuhusu usajili baada ya msimu kuisha ila nyota huyo yupo kwenye mipango yao.

"Ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa ambaye tungependa kuwa naye kwenye timu yetu,"