Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mo: Uwezo wa kushinda leo tunao

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Mohammed Dwji ‘Mo’ amewatia moyo wachezaji wa timu hiyo akisema kila kitu kinawezekana na kuwataka nyota hao kusaka pointi tatu mbele ya Al Ahly leo.

Akizungumza juzi wakati wa mazoezi ya mwisho ya kikosi cha Simba, Mo alisema kila kitu kinawezekana katika soka, huku akiwa na imani kubwa kuwa Simba itarudia kiwango zaidi ya kilichoonyeshwa wakati wakiilaza miamba hiyo kwa bao 1-0. Simba iliichapa Al Ahly katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja wa Mkapa kwa bao 1-0, ushindi uliochangia kuivusha timu hiyo katika hatua ya mtoano kabla ya kutolewa na TP Mazembe, mwaka juzi.