Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Coca Cola yazindua kampeni ya Kombe la Dunia 

UZINDUZI Pict

Muktasari:

  • Kampeni hiyo itashirikisha zaidi ya maduka 15,000 ya rejareja, migahawa, kumbi za burudani na vituo vya vyakula nchini kote. Ushiriki wa maeneo hayo unatarajiwa kutoa fursa kwa mashabiki kukutana, kufuatilia mechi na kusherehekea pamoja, huku ukichangia kuongeza shughuli za kibiashara katika kipindi cha mashindano.

KAMPUNI ya Coca Cola Tanzania imezindua kampeni ya kitaifa ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 inayolenga kuwaunganisha mashabiki wa soka nchini kupitia burudani, promosheni mbalimbali na shughuli za kidijitali zitakazowapa fursa ya kushiriki kwa karibu zaidi shamrashamra za michuano hiyo mikubwa zaidi duniani.

Kampeni hiyo, iliyoanza Juni 11 hadi Julai 19, 2026, inatarajiwa kuwafikia maelfu ya mashabiki wa soka nchini kupitia shughuli mbalimbali zitakazofanyika katika maeneo ya biashara, kumbi za burudani na majukwaa mbalimbali. Kupitia kampeni hiyo, kampuni hiyo inalenga kuhamasisha ushiriki wa mashabiki kupitia michuano ya Kombe la Dunia 2026.

Ikiwa ni sehemu ya ushirikiano wake wa takribani miongo mitano na FIFA, Coca-Cola inaendelea kutumia nguvu ya soka kuwaleta watu pamoja kupitia hisia, ushindani na furaha vinavyofanya Kombe la Dunia kuwa moja ya matukio makubwa zaidi ya michezo duniani.

Kampeni hiyo itashirikisha zaidi ya maduka 15,000 ya rejareja, migahawa, kumbi za burudani na vituo vya vyakula nchini kote. Ushiriki wa maeneo hayo unatarajiwa kutoa fursa kwa mashabiki kukutana, kufuatilia mechi na kusherehekea pamoja, huku ukichangia kuongeza shughuli za kibiashara katika kipindi cha mashindano.

Akizungumza kuhusu kampeni hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Coca-Cola Bonite Bottlers, Raman Anantha Narayanan, alisema soka lina nafasi ya kipekee katika kuunganisha watu kupitia uzoefu na hisia za pamoja.

"Soka ni zaidi ya mchezo; ni nguvu inayowaunganisha watu na jamii kupitia hisia za pamoja. Kupitia kampeni hii, tunalenga kuwapa mashabiki wa Tanzania fursa ya kushiriki kikamilifu msisimko wa Kombe la Dunia la FIFA 2026™ na kusherehekea pamoja kila hatua ya mashindano hayo," alisema.

Kwa mujibu wa Coca-Cola, kampeni hiyo itahusisha burudani mbalimbali, promosheni maalumu katika maeneo ya mauzo pamoja na kampeni za kidijitali zitakazowapa mashabiki nafasi ya kushiriki katika shughuli mbalimbali zinazohusiana na michuano hiyo.

Michuano ya Kombe la Dunia inafanyika kwa ushirikiano wa Marekani, Canada na Mexico ikiwa leo ni siku ya tatu tangu ilipoanza.