Baada ya kuiondosha Zalan FC ya Sudan Kusini kwa jumla ya mabao 9-0 katika mechi mbili nyumbani na ugeninini huku Fiston Mayele akitakata kwa kufunga hat-trick mara mbili, timu hiyo itakutana na kigogo kingine cha Sudan, Al Hilal yenye masikani yake katika mji wa Omdurman.
Hilal imefika hapo baada ya kuitoa Saint George ya Ethiopia kwa bao la ugenini baada ya kupoteza 2-1 ugenini na mechi ya pili kushinda 1-0 nyumbani.
Al Hilal inayonolewa na Kocha Florent Ibenge, haijawahi kabisa kukutana na Yanga kwenye michuano hiyo ya CAF, lakini zilishakutana mara tofauti katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), huku Yanga ikishinda mbili, ikipoteza mara moja na nyingine kuisha kwa sare.