USHINDI wa Argentina wa mabao 3-2 dhidi ya England jana jioni umeipa timu ya Taifa ya Walemavu ya Tanzania ‘Tembo Warriors’ nafasi ya kucheza hatua ya 16 bora ya Fainali za Kombe la Dunia nchini Uturuki.
Awali jana asubuhi Tembo waliifunga Uzbekistan mabao 2-0 na kulazimika kusubiri matokeo hayo ya jioni kujua hatma yao. Hiyo Tembo watacheza na Japan kesho Jumatano.