MAAFANDE wa Tanzania Prisons wapo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya pambano la Ligi Kuu Bara dhidi ya Yanga, lakini kabla ya pambano hilo linalopigwa leo Jumapili kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jamaa walitinga ofisi za wadhamini wao na baadaye wakaupiga ubweche kwa lengo la kupata ushindi.
Timu hizo zinakutana kuanzia saa 1:00 usiku, huku kila moja ikitoka kupata matokeo tofauti, vinara Yanga walipoteza mbele ya Ihefu mabao 2-1, Prisons ikitoka suluhu na KMC ndipo wakatinga Dar na kuzitembelea ofisi za wadhamini wao, Silent Ocean Ltd na Kilimanjaro Star Cargo.