Timu ya taifa Argentina imetinga nusu Fainali ya Kombe la Dunia 2022 baada ya kuiondoa Uholanzi kwa mikwaju ya penalti baada ya dakika 120 kumalizika kwa sare ya mabao 2-2.
Argentina imeshinda penalti 4-3 zikifungwa na Messi, Peredes, Montiel, Martinez huku Enzo Fernandez akipoteza.
Kwa upande wa Uholanzi penalti zao zimefungwa na de Jong, Weghorst, Koopmeiners huku van Dijk na Berghuis wakipoteza.
Argentina itakutana na Croatia katika hatua ya nusu Fainali ya kwanza Kombe la Dunia 2022, inayotarajiwa kuchezwa Desemba 14.