Simba iliyoiondosha Nyasa Big Bullets ya Malawi kwa jumla ya mabao 4-0, itakutana na Premiero De Agosto ya Angola iliyoiondosha Red Arrows ya Zambia kwa jumla ya mabao 2-1.
Agosto ina rekodi kubwa Afrika ikiwa imefika hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa mwaka 2018 kabla ya kuyumba miaka mitatu iliyofuata kutokana na Janga la Corona sasa imeanza kujijenga taratibu na kurejea kwenye ubabe wake.