Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wababe Simba walioichapa Yanga mara ya mwisho!

WABABE Pict


SIMBA imekubali vipigo sita mfululizo kutoka kwa Yanga, hali inayochangia Dabi ya Kariakoo kesho,  Jumapili kusubiriwa nini kitatokea. Wekundu wa Msimbazi wataendelea kuonewa au watakataa unyonge na kufungua ukurasa mpya.


Rekodi zinaonyesha, mara ya mwisho Yanga kupoteza mechi mbele ya Simba ilikuwa Agosti 13, 2023 katika mechi ya Ngao ya Jamii iliyochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.


Katika mechi hiyo, dakika 90 matokeo yalikuwa 0-0, penalti zikaamua ushindi kwa Simba ikiichapa Yanga 3-1, huku kipa Ally Salim akiibuka shujaa kwa kupangua mikwaju mitatu ya Khalid Aucho, Pacome Zouzoua na Yao Kouassi. 

Baada ya mechi hiyo, Yanga imetembeza vipigo sita mfululizo kwa Simba, vinne katika Ligi na viwili Ngao ya Jamii. 

Ubabe wa Yanga kwa Simba katika Ligi Kuu Bara matokeo yalikuwa hivi; Simba 1-5 Yanga (Novemba 5, 2023), Yanga 2-1 Simba (Aprili 20, 2024), Simba 0-1 Yanga (Oktoba 19, 2024) na Yanga 2-0 Simba (Juni 25, 2025). Pia mechi mbili za Ngao ya Jamii matokeo yali kuwa hivi; Yanga 1-0 Simba na Yanga 1-0 Simba.

Ukiangalia vikosi vilivyoanza katika mechi ile ya mwisho ambayo Simba inapata ushindi mbele ya Yanga na kulinganisha hivi sasa, kuna mabadiliko makubwa.

Kwa kukukumbusha tu, kikosi cha Yanga kilichoanza kilikuwa na; Djigui Diarra, Yao Kouassi, Joyce Lomalisa, Bakari Mwamnyeto, Ibrahim Bacca, Khalid Aucho, Maxi Nzengeli, Mudathiri Yahya, Clement Mzize, Kennedy Musonda na Jesus Moloko.

Benchi alikuwepo Metacha Mnata, Nickson Kibabage, Dickson Job, Gift Fred, Jonas Mkude, Salum Abubakar 'Sure Boy', Pacome Zouzoua, Aziz Ki na Hafiz Konkoni.

Kwa upande wa Simba, walioanza ni Ally Salim, Shomari Kapombe, Mohamed Hussein, Kennedy Juma, Che Malone Fondoh, Sadio Kanoute, Clatous Chama, Mzamiru Yassin, John Bocco, Saido Ntibazonkiza na Luis Miquissone.

Waliokuwa benchi ni Hussein Abel, Israel Mwenda, Hussein Kazi, Fabrice Ngoma, Aubin Kramo, Willy Onana, Moses Phiri, Kibu Denis na Jean Baleke.



Jina: Ally Salim

Nafasi: Golikipa

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: Dodoma Jiji


Jina: Shomari Kapombe

Nafasi: Beki wa kulia

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: Bado yupo Simba 


Jina: Mohamed Hussein

Nafasi: Beki wa kushoto

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: Yanga SC


Jina: Kennedy Juma

Nafasi: Beki wa kati

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: Singida Black Stars


Jina: Che Malone Fondoh

Nafasi: Beki wa kati

Uraia: Cameroon

Alipo sasa: USM Alger (Algeria)


Jina: Sadio Kanoute

Nafasi: Kiungo mkabaji

Uraia: Mali

Alipo sasa: Azam


Jina: Clatous Chama

Nafasi: Kiungo mshambuliaji

Uraia: Zambia

Alipo sasa: Amerudi Simba (aliondoka kwenda Yanga, kisha Singida BS) 


Jina: Mzamiru Yassin

Nafasi: Kiungo wa kati

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: TRA United (mkopo)


Jina: John Bocco

Nafasi: Mshambuliaji

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: Kocha wa vijana Simba


Jina: Saido Ntibazonkiza

Nafasi: Kiungo mshambuliaji

Uraia: Burundi

Alipo sasa: Vital'O FC (Burundi)


Jina: Luis Miquissone

Nafasi: Kiungo mshambuliaji

Uraia: Msumbiji

Alipo sasa: Al-Ahly SC (Libya)


Jina: Hussein Abel

Nafasi: Golikipa

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: Bado yupo Simba


Jina: Israel Mwenda

Nafasi: Beki wa kulia

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: Yanga SC


Jina: Hussein Kazi

Nafasi: Beki wa kati

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: Namungo


Jina: Fabrice Ngoma

Nafasi: Kiungo mkabaji

Uraia: DR Congo

Alipo sasa: Al-Nasr SC (Libya)


Jina: Aubin Kramo

Nafasi: Winga

Uraia: Ivory Coast

Alipo sasa: Ittihad Gharyan SC (Libya)


Jina: Willy Onana

Nafasi: Mshambuliaji

Uraia: Cameroon

Alipo sasa: CS Sfaxien (Tunisia)


Jina: Moses Phiri

Nafasi: Mshambuliaji

Uraia: Zambia

Alipo sasa: Green Eagles FC (Zambia)


Jina: Kibu Denis 

Nafasi: Mshambuliaji

Uraia: Tanzania

Alipo sasa: Al-Nasr SC (Libya)


Jina: Jean Baleke

Nafasi: Mshambuliaji

Uraia: DR Congo

Alipo sasa: Al-Khums SC (Libya)


KOCHA: Roberto Oliveira 'Robertinho'

Uraia: Brazil

Alipo sasa: Jeddah SC (Saudi Arabia)