Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Paten aumiza kichwa ujio wa wimbo mpya

PATEN Pict
PATEN Pict

Muktasari:

  • Ukiwa na wiki mbili tangu kuachiwa kwakwe katika majukwaa ya kuuza na kusikiliza muziki, wimbo huo unaendelea kupata mafanikio makubwa huku ukikubalika zaidi ndani na nje ya nchi.

MSANII anayetamba na kibao cha Afande, Dogo Paten amesema licha ya kwa sasa kuwa bize na kufanya shoo, pia anaumiza kichwa kutoa nyimbo nyingine zitakazopendwa kama ilivyo kwa wimbo huo.

Dogo Paten alipata maarufu wiki chache zilizopita baada ya Zuchu kuupenda wimbo wa Afande na kumsapoti kwa kufanya remix.

Akizungumza na Mwanaspoti, Paten alisema "Mimi ni msanii na siwezi kubweteka kwa sasa, siwezi kuharakisha kutoa ngoma lakini nakaa chini kuumiza niweze kuwalisha vitu vizuri mashabiki zangu," alisema Paten.

Ukiwa na wiki mbili tangu kuachiwa kwakwe katika majukwaa ya kuuza na kusikiliza muziki, wimbo huo unaendelea kupata mafanikio makubwa huku ukikubalika zaidi ndani na nje ya nchi.

Msanii huyo hivi karibuni amechaguliwa kuwania tuzo za ‘EAEA Awards’ kama Best Singeli Fusion kupitia wimbo huo.

"Sina mengi ya kusema kwa sababu hayo yote ni mipango ya Mungu, lakini nashukuru sana kwa kuchaguliwa na hilo linanifanya niendelee kupiga kazi kuhakikisha malengo yangu yanatimia."