Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Lil Jon apata pigo akifiwa na mwanae

LIL Pict

Muktasari:

  • Nathan aliripotiwa kutoweka Jumanne ya wiki iliyopita kabla ya juzi timu ya utafutaji ilipata mwili kutoka kwenye bwawa katika eneo hilo. Polisi wamesema hakuna dalili za uhalifu. Milton, Georgia iko takriban maili 30 kaskazini mwa Atlanta.

FLORIDA, MAREKANI: DJ Young Slade, mtoto wa nyota muziki wa Marekani, Lil Jon amefariki dunia, baba yake alithibitisha taarifa hiyo kupitia taarifa rasmi siku ya Ijumaa.

Lil Jon aliambia TMZ: “Nimevunjika moyo sana kwa kumpoteza mwana wetu kwa njia ya kusikitisha, Nathan Smith. Mama yake, Nicole Smith, na mimi tumehuzunika mno. Nathan alikuwa mtu mwema kuliko yeyote ambaye ungeweza kukutana naye. Alikuwa na moyo wa kujali sana, mwenye fikra, mwenye adabu, mwenye shauku, na mwenye upendo mwingi aliipenda familia yake na marafiki zake kwa dhati kabisa.”

Lil Jon aliongeza: “Alikuwa kijana mwenye kipaji cha ajabu; alikuwa mtayarishaji wa muziki, msanii na mhandisi wa sauti, na mhitimu wa Chuo Kikuu cha NYU. Tulimpenda Nathan kwa mioyo yetu yote na tunajivunia sana yeye. Alipendwa na kuthaminiwa, na katika nyakati zetu za mwisho pamoja tunapata faraja kujua kwamba tulimwambia wazi jinsi tulivyompenda.”

Rapa huyo pia aliishukuru Idara ya Polisi ya Milton kwa msaada wao katika juhudi za kumtafuta mwanawe.

Nathan aliripotiwa kutoweka Jumanne ya wiki iliyopita kabla ya juzi timu ya utafutaji ilipata mwili kutoka kwenye bwawa katika eneo hilo. Polisi wamesema hakuna dalili za uhalifu. Milton, Georgia iko takriban maili 30 kaskazini mwa Atlanta.

Mchunguzi wa maiti wa Kaunti ya Fulton aliambia TMZ kuwa chanzo na namna ya kifo cha Nathan bado havijabainika.