Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Babalevo aelezea ajali ya Shilole

SHILOLE Pict

Muktasari:

  • Akizungumza na Mwanaspoti, Mbunge wa Kigoma Mjini Baba Levo amesema, Shilole amepata ajali mbaya  hivyo anahitaji maombi apone haraka.

Msanii wa muziki Zuwena Mohammed maarufu kama Shilole amepata ajali ya gari akiwa njiani kwenda Dodoma kutoka mkoani Kigoma, alikokuwa ameshiriki katika shughuli ya kijamii iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Clayton Revocatus (Babalevo), iliyojulikana kama Pilau Day.


Akizungumza na Mwanaspoti, Mbunge wa Kigoma Mjini Baba Levo amesema, Shilole amepata ajali mbaya  hivyo anahitaji maombi apone haraka.

"Ni kweli Shilole amepata ajali, anahitaji maombi apone haraka, anaendelea kupata matibabu Tabora," amesema. 

Aidha kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii wa Instagram, Baba Levo amethibitisha tukio hilo akisema: “Jana usiku dada yangu Shilole alipokuwa anatoka Kigoma kurudi Dodoma alipata ajali ya gari aina ya Alphard baada ya kugonga ng’ombe maeneo ya Maragalasi. Tunafuatilia afya yake kwa ukaribu, kwa sasa anaendelea kupata matibabu Tabora.”


Mwanaspoti linaendelea kufuatilia zaidi, usikae mbali.