Aliyepora simu ya Mama Diamond akiona cha moto
Muktasari:
Mama mzazi wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi Sandra maarufu kama Mama Diamond amebiwa Simu katika Viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam.
MAMA mzazi wa staa wa kimataifa wa muziki wa kizazi kipya nchini, Diamond Platnumz, Bi Sandra maarufu kama Mama Diamond ameibiwa Simu katika Viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam, lakini aliyehusika na tukio hilo amekiona cha moto baada ya kushushiwa kipondo hevi.
Tukio hilo limetokea jioni ya janawakati wasanii wakiwa wanafanya Sound Check Kwenye Jukwaa La Wasafi festival kwa ajili ya Tamasha litakalo fanyika kesho Septemba 9, 2019.
Mama Diamond alifika katika viwanja hivyo akiwa ameongozana na mumewe Shamte na aliyekuwa Mkurugenzi wa African Stars 'Twanga Pepeta ' Asha Baraka, akiwa anashuka kwenye gari watu walimzunguka ndipo akatokea kijana mmoja alipomvamia na kumpora simu kisha kukimbia.
Kijana huyo hakupiga hatua hata kumi kabla ya kuvamiwa na kundi la watu na kuanza kumpiga baada ya kumnyang'anga simu na kama sio askari polisi waliomuokoa habari ingekuwa nyingine.
Baada ya hapo Mwanaspoti liliongea na Mama Diamond kuhusu tukio hilo, ambapo amesema, amejikuta amezungukwa na kundi la watu baada ya kufika katika eneo hilo na kuporwa simu na kijana huyo asiyemfahamu.
"Mimi hadi sasa sielewi, maana nimefika tu hapa, naona watu wamenizunguka kwenye gari yangu, nafungua mlango wamesogea ndipo yule kijana akanisogelea karibu yangu na kunipora simu," alisema Mama Diamond.
Hata hivyo Mama Diamond aliwaomba polisi wamsamehe kijana hiyo kwakuwa simu yake imerudi ila Polisi waligoma.