Sadney asawazisha bao

Dakika 29, Yanga ilipata bao baada ya beki Ally Ally kupiga krosi na kuchezwa na Patrick Sibomana na kuwa kona iliyopigwa na Sibomana na kukutana kiungo Abdulaziz Makame aliyepiga shuti na kutemwa na kipa wa Zesco.
Mpira huo ulikutana na Sadney Urikhoub aliyetuliza na kupiga shuti moja kwa moja na kutinga wavuni na kusawazisha bao kuwa 1-1 bao la Zesco lilifungwa na Jesse Were.