Man United kuja na mpango wa Haaland

Manchester United imejipa miezi 12 ya kumshawishi staa wa Borussia Dortmund na Norway Erling Braut Haaland ajiunge nao katika dirisha lijalo la ajira ya kiangazi.

Mchakato wa kuipata saini ya Haaland katika dirisha hili unaonekana kuwa mgumu baada ya Dortmund yenyewe kusisitiza kwamba haitomuuza. Mkataba wake unamalizika mwaka 2024.