Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Liverpool wanauliza, bado ngapi?

LIVERPOOL Pict

Muktasari:

  • Ushindi huo umeifanya Liverpool kufikisha pointi 70 na inahitaji kushinda mechi sita tu zijazo ili kutangazwa kuwa mabingwa wa msimu huu.

LIVERPOOL, ENGLAND: HESABU za ubingwa kwa Majogoo wa Jiji la Liverpool zinatoa matumaini katika kutwaa taji la Ligi Kuu England msimu huu baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Southampton juzi Jumamosi.

Ushindi huo umeifanya Liverpool kufikisha pointi 70 na inahitaji kushinda mechi sita tu zijazo ili kutangazwa kuwa mabingwa wa msimu huu.

Kwa sasa inaongoza kwa tofauti ya pointi 16 baada ya mechi 29  huku wapinzani wao wakubwa kwenye mbio hizo, Arsenal iliyopo nafasi ya pili ina mechi mbili mkononi.

Hata hivyo, sasa majogoo hawa  wanajua ni pointi ngapi wanahitaji kuhakikisha wanapata taji la ligi msimu huu.


Kiujumla vigogo hawa wanahitaji pointi 18 zaidi ili kuhakikisha wanapata taji ambao ni sawa na kushinda mechi sita zijazo hata kama Arsenal ikishinda mechi zao zote zilizobakia.

Ikiwa Arsenal itashinda mechi zote zilizobakia itafikisha a pointi 87, wakati Liverpool ikishinda mechi sita zijazo itakusanya jumla ya alama 88.

Kampeni yao ya kushinda mechi sita itaanzia mwezi ujao ambapo watacheza dhidi ya Everton katika dimba la Anfield April 02  baada ya Mapumziko ya kupisha kalenda ya FIFA.

Baada ya hapo wataumana na  Fulham ugenini April 6 kisha  West Ham nyumbani April 13, kisha watasafiri kwenda jijini  Leicester kuvaana na Leicester City  na baadae  wataikaribisha Tottenham ya Ange Postecoglou Anfiled.

Mchezo wa sita ambao watatakiwa kushinda baada ya kushinda mitano ya hapi juu ni dhidi ya Chelsea ambao utapigwa Mei 03 katika dimba la  Stamford Bridge.

Hata hivyo, kuna uwezekano wasishinde mechi hizo sita kwani na wakachukua ubingwa kwa kushinda tano au nne ingawa hiyo itategemea na matokeo ambayo Arsenal itakuwa inayapata.