Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Iran yajitoa Kombe la Dunia 2026

Muktasari:

  • Dunia ya mpira wa miguu inatarajiwa kukusanyika Amerika Kaskazini kwa ajili ya mashindano makubwa ya Kombe la Dunia majira ya kiangazi mwaka huu. Hata hivyo, waziri wa michezo wa Iran amethibitisha kuwa timu yao haitachukua nafasi yao katika mashindano hayo.

TEHRAN, IRAN: IRAN haitashiriki fainali za Kombe la Dunia 2026 kutokana na vita vinavyoendelea kati ya taifa hilo na Marekani, amesema waziri wa michezo wa nchi hiyo, Ahmad Donyamal.

Dunia ya mpira wa miguu inatarajiwa kukusanyika Amerika Kaskazini kwa ajili ya mashindano makubwa ya Kombe la Dunia majira ya kiangazi mwaka huu. Hata hivyo, waziri wa michezo wa Iran amethibitisha kuwa timu yao haitachukua nafasi yao katika mashindano hayo.

Ushiriki wa taifa hilo la Mashariki ya Kati ulikuwa tayari unahojiwa baada ya mashambulizi ya pamoja ya Marekani na Israel. Mashambulizi hayo yanadaiwa kumuua kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Khamenei, siku ya kwanza ya mashambulizi.

Waziri wa michezo Donyamal alisema kwenye televisheni: “Kwa kuwa serikali hii fisadi imemuua kiongozi wetu, hatuna mazingira yoyote ya kushiriki Kombe la Dunia. Kwa kuzingatia hatua ovu zilizochukuliwa dhidi ya Iran, vita viwili vimetulazimishwa ndani ya miezi nane au tisa, na maelfu ya watu wetu wameuawa. Kwa hiyo, hatuna kabisa uwezekano wa kushiriki kwa hali ilivyo sasa.”

Tangu mashambulizi ya kwanza ya Marekani na Israel, Iran imeripotiwa kujibu kwa mashambulizi dhidi ya vituo vya kijeshi vya Marekani katika nchi za Bahrain, Falme za Kiarabu (UAE), Oman, Saudi Arabia, Jordan, Qatar na Kuwait.

Kombe la Dunia linatarajiwa kufanyika Marekani, Canada na Mexico kuanzia Juni 11 hadi fainali Julai 19.

Iran ilipangwa kucheza na New Zealand na Belgium mjini Los Angeles kabla ya mchezo wao wa mwisho wa Kundi G dhidi ya Misri mjini Seattle. Hakuna timu iliyofuzu ambayo imejiondoa Kombe la Dunia tangu Ufaransa na India zilipojiondoa kwenye mashindano ya mwaka 1950 yaliyofanyika Brazil kwa sababu za gharama.

Iwapo Iran itajiondoa, FIFA itakabiliwa na changamoto ya kuamua ni timu gani itachukua nafasi yao, hasa kutokana na hali ngumu ya kisiasa katika Mashariki ya Kati. Jirani yao Iraq, ambayo imefuzu kukutana na Suriname au Bolivia katika mechi ya mchujo ya Inter-Continental huko Mexico baadaye mwezi huu, imeomba mchezo huo uahirishwe. Kocha Graham Arnold ana hofu kuhusu usalama wa wachezaji wake ikiwa watalazimika kusafiri kwa basi kwa safari ya saa 25 kwenda Uturuki.

Chaguo moja linaweza kuwa kuruhusu Iraq kuchukua moja kwa moja nafasi ya Iran, huku mchezo kati ya Suriname na Bolivia ukiwa wa kuamua nani aingie Kombe la Dunia. Au kama mechi za mchujo zitaendelea na Iraq ikashinda, FIFA inaweza kupandisha Falme za Kiarabu (UAE), ambao ni timu inayofuata kwa ubora katika Asia.

Kujiondoa kwa Iran kunakuja wakati rais wa FIFA, Gianni Infantino alisema kuwa rais wa Marekani Donald Trump amedai kuwa Iran “wanakaribishwa” kushiriki. Hii ni licha ya Trump kusema pia wiki iliyopita kuwa “sijali sana” kuhusu ushiriki wa Iran alipoulizwa na Politico.

Infantino alisema katika taarifa: “Jioni hii nilikutana na Rais wa Marekani Donald J. Trump kujadili maandalizi ya Kombe la Dunia la FIFA lijalo na msisimko unaoongezeka huku tukibakiza siku 93 kabla ya kuanza. Pia tulizungumza kuhusu hali ya sasa nchini Iran na ukweli kwamba timu ya Iran imefuzu kushiriki Kombe la Dunia la FIFA 2026.

“Katika mazungumzo hayo, Rais Trump alisisitiza kwamba timu ya Iran, bila shaka inakaribishwa kushiriki katika mashindano hayo nchini Marekani. Sote tunahitaji tukio kama Kombe la Dunia kuwaleta watu pamoja zaidi kuliko wakati mwingine wowote na ninamshukuru sana Rais wa Marekani kwa msaada wake, kwani inaonyesha tena kwamba mpira wa miguu unaunganisha dunia.”

Iran ilipata nafasi yao katika mashindano hayo baada ya kumaliza nafasi ya kwanza katika Kundi A la kufuzu Kombe la Dunia 2026 kwa ukanda wa Asia.