Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Pale kwa Bangala panamfaa Kanoute

Yanga wanalazimika kusajili kiungo mkabaji kwenye dirisha hili endapo kiungo wao mahiri Yanick Bangala ataondoka kwenye timu hiyo.

Siku chache kabla msimu haujamalizika, Kanoute alinukuliwa akisema kuwa mkataba wake na Simba umemalizika na katika mazungumzo yao hawajafikia muafaka.

Huyu ni kati ya viungo mahiri wageni ambao wameonyesha kiwango cha juu kwa kipindi chote alichotumika kwenye kikosi cha Simba, akiwa anatajwa kuwa mmoja kati ya wachezaji wasomi zaidi hapa nchini.

Kanoute raia wa Mali anaweza kuwa msaada sahihi kwa Yanga kwenye eneo la kiungo kama watazungumza naye akiwa na uzoefu mkubwa kwenye ligi kuu, tofauti na yule atakayekuja na asubiriwe hadi azoee, lakini atapunguza gharama kwao kwa kuwa atapatikana bure sokoni.