Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Hii ya Yanga haijawahi tokea

Muktasari:

Amissi Tambwe amepiga bao tatu na kuandika ‘hat trick’ yake ya kwanza msimu huu akimjibu Ibrahim Ajibu wa Simba aliyekuwa pekee mwenye idadi hiyo.

SIKIA hii, Jana Jumatano ilikuwa Aprili 8 na Yanga ilichofanya ni kumpiga mtu mabao nane Uwanja wa Taifa. Kipigo hicho ilichotoa Yanga kwa Coastal Union inayofundishwa na kocha mwenye maneno mengi na mikwara ya kufa mtu, Jamhuri Kihwelu ‘Julio’ hakijawahi kuikumba timu yoyote ya Bongo ndani ya miaka 10 iliyopita.

Amissi Tambwe amepiga bao tatu na kuandika ‘hat trick’ yake ya kwanza msimu huu akimjibu Ibrahim Ajibu wa Simba aliyekuwa pekee mwenye idadi hiyo.

Hali ikiwa hivyo kwa Yanga, mabingwa watetezi Azam walishindwa kutamba nyumbani baada ya kung’ang’aniwa na Mbeya City na kutoka sare ya 1-1 katika pambano jingine la ligi hiyo jana.

Yanga ilipata ushindi huo mnono na kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wakiwa na pointi 43 baada ya mechi 20.

Tambwe aliyefunga mabao manne, alianza kuandika bao la kuongoza dakika ya 10 akiunganisha pasi ya kichwa ya Kpah Sherman baada ya mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na beki Oscar Joshua.

Simon Msuva alifunga bao lake la 12 katika Ligi Kuu msimu huu baada ya kuwafunga tela mabeki wa Coastal na kuifungia Yanga bao la pili dakika ya 24.

Wakati Coastal wakijiuliza huku wakifanya kosakosa za hapa na pale na kupoteza nafasi za wazi, Tambwe alirudi tena kambani kwa kufunga bao la tatu dakika ya 35 kutokana na kuunganisha shuti la Juma Abdul. Matokeo yalikuwa mabao 3-0, Yanga wakiongoza hadi wakati wa mapumziko.

Kipindi cha pili kilianza kwa Coastal kufanya mabadiliko ya kumtoa Rama Salim na kumuingiza Athuman Abussi, mabadiliko ambayo hayakuwatisha Yanga kwani Tambwe alifunga bao lake la tatu katika mechi hiyo na la nne kwa Yanga katika dakika ya 48 akimaliza pasi nzuri ya Msuva.

Dakika ya 50 Mliberia Kpah Sherman aliondoa ‘gundu’ la miezi minne Yanga bila kufunga baada ya kuunganisha krosi ya Tambwe na kuiandikia Yanga bao la tano. Msuva alifunga bao lake la 13 dakika za 86 akiunganisha krosi ya Tambwe na Salum Telela aliongeza la saba la Yanga dakika ya 88 kabla ya Tambwe kufunga bao lake la nne na la nane kwa Yanga katika pambano hilo ambalo Coastal ilifunikwa kabisa Taifa.

YANGA: Barthez, Juma Abdul, Oscar Joshua/ Edward Charles, Cannavaro, Yondani, Twitte/Dilunga, Telela, Niyonzima, Tambwe, Sherman/ Nizar Khalfan na Msuva.

COASTAL: Fikirini Bakar, Juma Hamad, Mfuko Abdallah, Chuma Yusuf, Mtama Bakar, Abdulhalim Humud, Mohammed Ally, Yahya Ayoub, Rajab Mohammed/Sekuhe Mohammed, Bright Obinna/Mtindi Mohammed na Rama Salum/Athuman Abussi

Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, mabingwa watetezi Azam waling’ang’aniwa na Mbeya City kwa sare ya 1-1 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

Azam ilipata bao dakika ya 61 kupitia kwa kiungo Kipre Balou aliyepiga shuti kali nje ya 18 akiunganisha krosi ya Pascal Wawa.

Wagonga Nyundo wa Mbeya, walisawazisha dakika tatu baadaye kupitia kwa Raphael Alfa kwa penalti baada ya Erasto Nyoni kumchezea madhambi Deud Kaseke.

Mara baada ya mechi hiyo ya Chamazi, viongozi wa Azam, meneja Jemedari Said na Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, Saad Kawemba walishikana mashati wakitaka kupigana kabla ya kuamuliwa na polisi waliokuwa wakilinda usalama. Haikuweza kufahamika mara moja kisi cha wawili hao kutunishiana misuli, ingawa inadaiwa matokeo hayo ni chanzo cha mzozo huo.