Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Crows yaanza visingizio

Muktasari:

  • Timu hiyo ilipoteza mchezo huo wa Ligi ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BDL) uliopigwa kwenye Uwanja wa DonBosco Oysterbay.

CROWS imeanza visingizio baada ya kocha wa timu hiyo, Abbas Sanawe kusema kuwa, kukosa utulivu kwa   wachezaji hasa katika robo ya tatu, imechangia kwa kiasi kukikubwa kufungwa na Savio kwa pointi 92-70.

Timu hiyo ilipoteza mchezo huo wa Ligi ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BDL) uliopigwa kwenye Uwanja wa DonBosco Oysterbay.

Sanawe aliliambia Mwanasposti kuwa, kukosa utulivu huo ilisababisha waweze kupoteza mipira mara kwa mara katika robo hiyo.

"Kuona hivi wapinzani wetu  walitumia nafasi hiyo ya uzembe tuliofanya kufunga pointi mara kwa mara na kuzidi ujanja," alisema Sanawe. 

Hadi kufikia mapumziko Savio walikuwa mbele kwa pointi 44-42.

Akizungumza mkakati waliouweka baada ya kupoteza mchezo  huo, alisema kwa sasa wamejipanga kushinda michezo  yote iliyokuwa mbele yao.

"Tukishinda baadhi ya michezo naamini tutashika nafasi ya nzuri   itakayotufanya tucheze ligi tena mwakani," alisema Sanawe