Mbao yaingia kimyakimya, Simba shangwe Kirumba
Muktasari:
Mbao iwapo itashinda mchezo huo itapanda hadi kukaa kileleni mwa Ligi Kuu Bara
T: Mbao yaingia kimyakimya, Simba shangwe Kirumba
S: Mbao iwapo itashinda mchezo huo itapanda hadi kukaa kileleni mwa Ligi Kuu Bara
Mwahiba Richard
Mwanza. Mbao FC imefika uwanjani saa 8:18 mchana ikiitangulia Simba iliyoingia saa 8:57 tayari kwa mechi yao itakayoanza saa 10:00 jioni kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Mashabiki wa Simba waliokaa eneo la vyumba vya kubadilishia nguo wachezaji waliishangilia timu yao kwa nguvu tofauti na ilivyoingia Mbao wenyeji, lakini ina mashabiki wachache.
Mbao iliongozwa na magari mawili madogo wakati Simba iliongozwa na gari la Polisi wa kuzuia ghasia (FFU). Timu zote zimeingia mlango mkubwa wa magari na kuingia vyumbani.
Hata hivyo, mpaka muda huu mashabiki ni wachache ingawa bado wanaendelea kuingia.
Vikosi
Mbao: Hashim Mussa, Vicent Philipo, Amos Charles, David Mwassa, Peter Mwangosi, Ally Mussa, Said Khamis, Hussein Seleman, Rajesh Kotecha, Pastory Athanas na Aboubakary Mfaume.
Benchi: Bruno Thomas, Hamimu Abdul, Yusuph Amos, Evarijestus Mujwahuki, Zamfuko Elias, Roland Msonjo na Emmanuel Mtumbuka
Simba: Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohammed Hussein, Erasto Nyoni, Pascal Wawa, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Clatous Chama, John Bocco, Emmanuel Okwi na Mohammed Ibrahim
Akiba: Deogratius Munish, Paul Bukaba, James Kotei, Said Ndemla, Meddie Kagere, Marcel Bonaventure.
Waamuzi: Waamuzi: Mbao vs Simba Katikati: Jonesia Rukyaa (Kagera), R1: Makame Mdogo (Shinyanga), R2: Martin Mwalyaje (Shinyanga)