TIMU ya DTB imefanikiwa kupanda Ligi Kuu Bara msimu ujao baada ya leo kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Pamba, mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi.
Bao la timu hiyo lilifungwa na Joel Madondo dakika ya 75, aliyeingia kipindi cha pili akichukua nafasi ya Tafadzwa Kutinyu ambaye hakuwa na mchezo mzuri.
DTB inashika nafasi ya kwanza na pointi 65 baada ya kucheza michezo 28, ikishinda 20, sare tano na kufungwa mitatu, huku Pamba inasalia nafasi ya tisa na pointi 36, baada pia ya kucheza michezo 28.