Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ibenge kasukuma kete za ushindi Azam

IBENGE Pict

Muktasari:

  • Baada ya wiki mbili za kusambaa kwa taarifa za Ibenge kukaribia kuwa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Mali, Azam wamezika rasmi tetesi hizo kwa kufichua kocha huyo atakuwepo hadi 2028.

ZILE tetesi za Florent Ibenge kuondoka Azam FC sasa zimezikwa rasmi na hatimaye Kocha huyo raia wa DR Congo sasa atabakia rasmi klabuni hapo.

Baada ya wiki mbili za kusambaa kwa taarifa za Ibenge kukaribia kuwa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Mali, Azam wamezika rasmi tetesi hizo kwa kufichua kocha huyo atakuwepo hadi 2028.

Kwa sisi tuliosoma Cuba hapa kijiweni, tunaona kama taarifa za Ibenge kukaribia kujiunga na timu ya taifa ya Mali hazikuibuka kwa bahati mbaya na wala siyo jambo hilo halikuwa na ukweli.

Inavyoonekana ni kweli Ibenge aliomba kazi ya kuinoa Mali na ndiyo maana baada habari ya kuongeza mkataba wa kuitumikia Azam FC inaonekana kuwavuruga sana mabosi wa chama cha soka Mali.

Hapo kwenye kuomba, tunahisi kuna sababu moja hivi ya msingi ambayo imepelekea kocha wa mpira Ibenge kufanya jambo kimyakimya kwa kutuma maombi ya kazi kuinoa  Mali pasipo kuwajuza waajiri wake.

Sababu hiyo ni kutengeneza mazingira ya kupata ongezeko la fedha katika mkataba wake kama ambavyo tunahisi bila kufanya hivyo pengine mambo yanakuwa hayaendi vyema.

Kama kusingekuwa na hiyo hali ya kuviziwa na chama cha soka Mali, pengine Azam FC wasingeona haja ya kumuongezea mkataba mpya kocha huyo kwa sasa kama ambavyo tayari wamefanya.

Pia imemsaidia Ibenge kufahamu nafasi na hadhi yake ndani ya klabu hiyo. Kuona maofisa wa Azam FC hawapati nafasi ya kupumua ili kuhakikisha suala la kocha huyo kutimkia Mali halizai matunda.