Noma sana, Arsenal yapewa Man City

LONDON, ENGLAND. ARSENAL itakipiga na Manchester City kwenye robo fainali ya Kombe la Ligi baada ya kuwachapa Liverpool kwa penalti. Kocha Mikel Arteta atakabiliana na bosi wake wa zamani Pep Guardiola huko Emirates. Arsenal ilipata sare ya bila kufungana na Liverpool kabla ya kushinda penalti 5-4. Everton walio kwenye ubora wao watacheza na Manchester United uwanjani Goodison Park. Ushindi wa Stoke City dhidi ya Aston Villa na sasa watakipiga na Spurs kwenye robo fainali.

Brentford, ambao waliipiga Fulham 3-0, watakipiga na Newcastle United kwenye uwanja wao mpya. Mechi zitapigwa Desemba.