NBA kurejea na mashindano ya timu 22 kuhitimisha msimu wa 2019-20

Msimu wa NBA wa 2019-20 utarejea tena Julai 31 wakati timu 22 zitakapokuwa zikishindana katika mashindano yanayofanyika huko Orlando, Florida kumaliza kampeni. Kuendelea kwa msimu huo kuliidhinishwa na makubaliano na wamiliki wa timu na huku kukiwa na klabu moja tu iliyopiga kura ya hapana dhidi ya kurejea kwa msimu, ambayo ni Portland Trail Blazers.
Msimu wa NBA ulisimama mwezi Machi na kwa wakati unarudi, itakuwa umesimamishwa kwa zaidi ya miezi nne. Mashabiki wa mpira wa kikapu wanatarajia kurudi kwa Chama na mashindano ya timu 22 yatakayomtafuta na kumtanganza bingwa. Mashindano hayo ya mpira wa kikapu huko Orlando si mashindano pekee ya mchezo wa kulipwa yanayofanyika katika Jiji hilo, kulingana na Real Soccer 365, Ligi kubwa za kabumbu pia zinaweza kurejea  kwenye jiji hilo na kuhitimisha mashindano kwa kutumia muda mfupi. Mashindano ya NBA yatafanyika kwenye Hoteli ya Walt Disney World ambayo yatakwenda mpaka Oktoba.
Hivyo, ni namna gani NBA itamaliza kampeni ya 2019-20 na kumvisha taji bingwa mpya?

Kumvisha taji bingwa wa NBA
Mpango wa NBA unaweza kuonekana mgumu kutekelezeka kiuhalisia, lakini utahitimisha kampeni iliyopo kwa kumvika taji bingwa mpya. Mashindano hayo yanaweza kushuhudia timu isiyotarajiwa ikinyakua mpja ya tuzo kubwa za NBA. Chini ya muundo wa mashindano hayo, kulingana na ripoti za hivi punde, timu 13 kutoka Upande wa Magharibi zitaungana na vilabu tisa vya Upande wa Mashariki. Timu hizo zitashindana katika michezo nane kumaliza msimu wa kawaida. Msimamo wa mwisho utatoa matokeo kwa ratiba za michezo ya mtoano.


Bodi ya Magavana ya NBA iliidhinisha muundo wa mashindano na ikachagua timu nane za juu katika kila upande kushindana. Timu sita zingine zaidi ziliongezwa kwenye mashindano kulingana na uwezekano wao wa kubakia kwenye mashindano ya NBA kwa msimu ujao kama msimu ule usingesimama. Timu sita za ziada zilichaguliwa kwa sababu walikuwa na michezo sita au michache nyuma ya kundi la nane kwenye aidha Upande wa Mashariki au Magharibi.
Mashindano hayo yatawapa mashabiki nafasi ya kutazama idadi ya michezo ya NBA kwa siku. Mara mashindano yatakapoanza katika hoteli ya Walt Disney, michezo mitano hadi sita itafanyika. NBA itatumia viwanja vitatu tofauti kwenye mashindano hayo na masaa manne tu yatatenganisha baina ya kila michezo kwa kila siku.

Timu zote za NBA zitawasili Orlando kwenye Hoteli ya Walt Disney Julai 9 kuanza mazoezi. Michezo itaisha mnamo Julai 31 na msimu uliorejea utakwenda kumalizika tena hadi Oktoba 12. Muendelezo wa msimu wa 2019-20 unaweza kuuweka msimu ujao katika mashaka, hata hivyo, NBA imetangaza  kuanza kwa kampeni ya 2020-21.
Msimu ujao katika NBA utakuaje?
Msimu huu wa NBA ulitakiwa uwe umemalizika hadi sasa huku shughuli zote za usajili wa wachezaji yanaendelea na wachezaji walio huru kuamua hatima zao. Kadhia ambayo haikutarajiwa iliyosababisha kusimama kwa msimu utalazimisha shughuli hizi zifanyike sasa Oktoba baada ya kukamilika kwa mashindano ya timu 22 ya NBA.
Oktoba 15 imechaguliwa kuwa kama Siku ya usajili wa wachezaji wa NBA wakati timu za ligi zitakapo kuwa zinachagua wachezaji bora wa mpira wa kikapu kutoka katika vyuo kujaza nafasi ya kucheza msimu ujao. Kipindi wachezaji kumaliza mikataba yao kinadaiwa kuanza Oktoba 18 na kambi kwa ajili ya mazoezi itaanza Novemba 10. Mapumziko ya kumalizika kwa msimu wa 2019-20 na 2020-21 yatastahili kufupishwa kwani mipango ya NBA ya kuanza msimu ujao Disemba 1.