Mkongo ataja mambo matano

KOCHA Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera ameamua kuanika mambo matano aliyonayo Ibrahim Ajibu, huku akisisitiza bado hajaridhika naye licha ya kuibeba timu kwa sasa.

Mkongomani huyo alisema jambo la kwanza ni kwamba Ajibu ni mchezaji wa tofauti wa aina yake na ana kipaji kikubwa cha soka na kabla hajapasiwa mopira hujua wapi pa kujipanga tofauti na wenzake.

Pia alisema anatengeneza nafasi za kufunga na kudai nafasi nane alizotengeneza mpaka sasa katika mechi zao saba ni chache na ataendelea kumpa mbinu nyingi mazoezini ili atishe zaidi ya hapo.

“Jambo la tatu kwa Ajibu ni kupata nafasi ya kucheza timu ya Taifa, nafasi hiyo inawezekana kutokana na kiwango chake ambacho anaonesha katika ligi kwa sasa lakini linaweza kuwa gumu kama hataonyesha uwezo wa kumshawishi kocha.”

Ajibu pia bado anakosa ujanja wa kutumia nguvu na huwa namwambia mara kwa mara uwezo wa kucheza mpira anao ila hana nguvu na anapaswa kuongeza kwa kufanya mazoezi ya nguvu lakini naona bado hajafanya hilo.

“Mwisho Ajibu akiongeza umakini zaidi ya sasa naona akifika mbali katika soka na kuwa na mafanikio mengi na hata kucheza soka Ulaya na kuitwa Stars itakuwa kama mtu kumeza mate.”