Mastaa Ulaya wamfariji Welback
Muktasari:
Kiungo huyo ambaye kwa sasa anaichezea Villarreal ya Hispania amemtakia apone haraka kupitia mtandao wake wa kijamii wa Istagram baada ya mshambuliaji huyo kuumia kwenye mchezo uliomalizika kwa suluhu.
BAADA ya Danny Welbeck wa Arsenal kumia vibaya jana kwenye mchezo wa Europa Ligi dhidi ya Sporting Lisbon, kiungo wa zamani wa timu hiyo, Santi Cazorla ametopa pole kwa mshambuliaji huyo.
Kiungo huyo ambaye kwa sasa anaichezea Villarreal ya Hispania amemtakia apone haraka kupitia mtandao wake wa kijamii wa Istagram baada ya mshambuliaji huyo kuumia kwenye mchezo uliomalizika kwa suluhu.
Maneno hayo yalikuwa yakisomeka: “Pona haraka rafiki yangu. Kuna vitu vingi vya thamani kwenye soka lakini natambua kuwa kuwa wewe ni shupavu na utapona haraka,kila la kheri mtu wangu.”
Welbeck alipata majeraha hayo dakika ya 30 ya mchezo huo baada ya kashikashi za kuucheza mpira kwa kichwa.
Summary
Welbeck amekuwa na historia ya kupata majeraha ya mara kwa mara, mshambuliaji huyo anakumbukwa kwa kuikosa kwake michuano ya mataifa ya Ulaya, 2016 kutokana na majeraha aliyoyapata akiwa na Arsenal.