Mane, Koulibaly kuiongoza Senegal Afcon

Muktasari:

Senegal imepangwa Kundi C pamoja na Algeria, Kenya, na Tanzania. Simba wa Teranga wataongozwa na mshambuliaji wa nyota wa Liverpool, Sadio Mane na beki Napoli, Kalidou Koulibaly.

Cairo, Misri. Kocha wa Senegal, Aliou Cisse ametangaza kikosi kilichojaa nyota 23, tayari kwa fainali za Mataifa ya Afrika yatakayofanyika Misri.

Kikosi hicho ni moja ya kikosi bora zaidi katika magazeti kutokana na kuundwa kwa nyota wengi, Senegal pia imeita wachezaji wanaotegemewa kuwika zaidi baada ya fainali za Misri.

Senegal imepangwa Kundi C pamoja na Algeria, Kenya, na Tanzania. Simba wa Teranga wataongozwa na mshambuliaji wa nyota wa Liverpool, Sadio Mane na beki Napoli, Kalidou Koulibaly.

Kikosi:

Makipa: Abdoulaye Diallo, Alfred Gomis, Edouard Mendy

Mabeki: Moussa Wague, Pape Abou Cisse, Salif Sane, Youssouf Sabaly, Lamine Gassama, Kalidou Koulibaly, Saliou Ciss, Cheikhou Kouyate

Viungo: Alfred N’diaye, Santy Ngom, Idrissa Gana Gueye, Krepin Diatta, Pape Alioune Ndiaye, Sidy Sarr, Henri Saivet

Washambuliaji: Ismaila Sarr, Keita Balde, M’Baye Niang, Moussa Konate, Mbaye Diagne, Sada Thioub, Sadio Mane.