La Liga kurejea kwa kishindo mubashara kupitia DStv

Baada ya mapumziko ya takribani mwezi mmoja tangu kumalizika kwa msimu wa soko kwenye mataifa mbalimbali barani Ulaya, ligi mbalimbali barani humo zimeanza na nyingine zinatarajia kuanza kutimua vumbi hivi karibuni.

Miongoni mwa nchi ambazo ligi zinatarajiwa kuanza ni Hispania ambayo ligi kuu nchini humo maarufu kama La Liga inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 11 kwa mchezo kati ya Granada watakao wakaribisha Athletic Club kwenye dimba la Estadio Nuevo Los Caemenes.

Je, Messi na Barcelona yake chini ya kocha mpya Ronald Koeman wataweza kuizuia Real Madrid kutetea ubingwa wake? Je Zidane ataendeleza ubabe na moto aliouwasha msimu uliopita kwenye La Liga? vipi kuhusu vijana wa Diego Simeone (Atletico Madrid) na je vipi kuhusu mabingwa wa Europa Sevilla?  

Yote haya utayashuhudia moja kwa moja (Live) kwenye kisimbuzi (decoder) chako pendwa cha DStv kupitia chaneli ya Supersport kwa gharama ya Sh 19,900 pekee kwa kifurushi cha Bomba ambacho kinakuwezesha kutazama zaidi ya chaneli 75 ikiwemo chaneli ya SuperSport La Liga.

Lipia sasa kisimbuzi chako ili usipitwe na uhondo huu wa soka kupitia DStv kwa kupiga *150*53# au tembelea tovuti yetu ya www.dstv.com.