Kocha Simba amweka benchi Okwi
Muktasari:
Kocha Mkuu wa Simba, Mbelgiji Patrick Aussems amekifanyia mabadiliko kikosi chake kitakachoivaa Mwadui FC leo Jumapili na miongoni mwa wachezaji aliowapumzisha ni Emmanuel Okwi.
Shinyanga. Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amesema, kutomtumia mshambuliaji wake, Emmanuel Okwi raia wa Uganda ni sehemu ya mipango yake ya ushindi.
Mechi iliyopita, Aussems alimwanzisha Okwi kwenye kikosi cha kwanza lakini mara kadhaa mashuti yake yaliyolenga golini hayakumpa matokeo mazuri wakafungwa na Mbao FC bao 1-0, mchezo uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Aussems amesema, ana wachezaji wazuri wengi anaowaamini na baada ya kuuangalia Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga amegundua si rafiki kwao ndiyo maana akafanya mabadiliko hayo.
Katika kikosi chake kitakachoivaa Mwadui FC leo Jumapili ya Septemba 23, Mghana James Kotei ameanza kikosi cha kwanza wakati mechi iliyopita alikuwa benchi.
Mnyarwanda Meddie Kagere aliyeanzia benchi mechi ya Mbao FC ameanza huku Mohammed Ibrahim 'Mo Ibrahim' akianzia benchi.
KIKOSI CHA SIMBA
Aishi Manula
Mohammed Hussein
Shomary Kapombe
Erasto Nyoni
Paschal Wawa
Jonas Mkude
James Kotei
Cletus Chama
John Bocco
Meddie Kagere
Shiza Kichuya
WA AKIBA
Deogratius Munish 'Dida'
Paul Bukaba
Emmanuel Okwi
Adam Salamba
Mohamed Ibrahim
Rashid Juma