Biashara yajifua kuikabili Yanga
Muktasari:
Kikosi cha klabu ya Biashara Utd, kimetua Jijini Dar es salaam na tayari kimeanza mazoezi kwaajili ya kuwakabili Yanga
Jumapili.
KIKOSI cha klabu ya Biashara Utd kimetua jijini Dar es Salaam na
kuanza mazoezi kwaajili ya kuwakabili wapinzani wao Yanga siku ya Jumapili.
Biashara itakuwa wageni kwa Yanga katika mchezo utakaopigwa Jumapili kwenye uwanja wa Taifa.
Mazoezi hayo yakisimamiwa na kocha Aman Josiah, walianza kwa kupasha misuli
kwa staili ya aina yake baada ya kucheza safa bwege na sio kukimbia raundi nyingi.
Imezoeleka kuonakana kwamba timu nyingi
wamekuwa wakikikbia sana pindi wanapoanza mazoezi lakini imekuwa tofauti katika mazoezi ya klabu ya Biashara.