Biashara yajifua kuikabili Yanga

Muktasari:

Kikosi cha klabu ya Biashara Utd, kimetua Jijini Dar es salaam na tayari kimeanza mazoezi kwaajili ya kuwakabili Yanga

Jumapili.

KIKOSI cha klabu ya Biashara Utd kimetua jijini Dar es Salaam na

kuanza mazoezi kwaajili ya kuwakabili wapinzani wao Yanga siku ya Jumapili.

Biashara itakuwa wageni kwa Yanga katika mchezo utakaopigwa  Jumapili kwenye uwanja wa Taifa.

Mazoezi hayo yakisimamiwa na kocha Aman Josiah, walianza kwa kupasha misuli

kwa staili ya aina yake baada ya kucheza safa bwege na sio kukimbia raundi nyingi.

Imezoeleka kuonakana kwamba timu nyingi

wamekuwa wakikikbia sana pindi wanapoanza mazoezi lakini imekuwa tofauti katika mazoezi ya klabu ya Biashara.