Failuna ashinda mbio za nyika Taifa

Muktasari:

Wanariadha 24 wataingia kambini kuwakilisha nchi katika mashindano ya mbio za dunia za nyika mapema mwezi Machi nchini Denmark.

Kilimanjaro. Mwanariadha Tanzania, Failuna Matanga ameshinda mashindano ya mbio za Nyika Taifa akitumia muda wa dakika 34:55 katika umbali wa kilomita 8 leo Jumamosi mkoani Kilimanjaro.

Mashindano hayo yalifanyika kwenye viwanja vya Gofu mjini Moshi, nafasi ya pili imeenda kwa mwanariadha Magnalena Shauri aliyetumia dakika 35:20 huku nafasi ya tatu akichukua Angelina Daniel Tsere aliyetunia dakika 36:45.

Nafasi ya nne imechukuliwa na Amina Mohamed (37:12), akifuatiwa na Marselina Issa (38:04) huku wa sita akichukua Rosalia Fabian (38:24).

Washindi sita wamechaguliwa kuingia kambini katika kambi ya taifa inayojiandaa na mashindano ya dunia ya mbio za nyika nchini Denmark.