Try Again: Mo Dewji alinipigia simu!

Muktasari:

Kiongozi wa juu wa Simba, Salim Abdallah 'Try Again' amewataka Watanzania na wadau wa Simba kutulia kutokana na tukio la kutekwa kwa mwanachama wa klabu hiyo, Mohammed Dewji 'Mo Dewji' kwa sababu suala hilo liko chini ya jeshi la polisi.

Cape Verde: Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah 'Try Again' amewaambia mashabiki wa klabu hiyo kutulia baada ya tukio la mwanachama mwenzao, Mohammed Dewji 'Mo' kutekwa na ameweka wazi kuwa alimpigia simu kabla ya tukio.
Try Again ni miongoni mwa wadau waliokwenda nchini Cape Verde kwa ajili ya kuiunga mkono timu ya Taifa Stars.
Alisema, tukio hilo ni la kusikitisha na amewaomba Watanzania hususani wanachama wa Simba watulie.
"Jambo linalotakiwa kufanywa sasa ni kumwombea dua, ili mwenzetu awe salama huko alipo na jeshi la polisi linafuatilia kwa ukaribu suala hilo,"alisema Try Again.
Amefafanua kuwa, jana Jumatano, Mo alimpigia simu kuomba mawazo kwake na wakaongea kwa kipindi kirefu.
"Alikuwa na kikao cha bodi na kuna mambo aliomba nimshauri, lakini ndiyo hivyo tena," alifafanua.
Namna alivyowatuliza wachezaji wa Simba ambao wako na Taifa Stars nchini Cape Verde.