Beka Mfaume aibuka na Jeraha la Mwiba

VIDEO: BEKA MFAUME AIBUKA NA JERAHA LA MWIBA

BAADA ya kutamba na riwaya kali na za kusisimua za Mwanamji na Siku ya Utakaso zilizochapishwa kwenye gazeti bora la michezo na burudani kwa Ukanda wa Afrika Mashariki, Mwanaspoti.
Gwiji la riwaya nchini, Beka Mfaume sasa anakuja na kitu kingine kitamu zaidi kinachokwenda kwa jina la Jeraha la Mwiba.
Hii ni riwaya mpya kabisa yenye visa vya mapenzi, huzuni, umafia na mambo ambayo yameshika hatamu kwenye jamii zetu.
Hakikisha unaungana naye ndani ya Gazeti la Mwanaspoti kuanzia Jumamosi ya Desemba 5, 2020.