Billnas, Nandy kuna jambo

MOJA ya couple za Tanzania zinazonogesha Instagram kwa mapicha picha ya mahaba ni ya rapa Billnas na African Princess, Faustina Mfinanga maarufu Nandy.

Sasa sikia, hivi tunavyozungumza kuna dalili kwamba penzi la wawili hao tayari limeingia mdudu-kuachana. Dalili ya kwanza ni majuzi, Nandy alipost picha ya ua jeusi kwenye akaunti yake Instagram, ua ambalo mara nyingi limekuwa likiashiria kuvunjika kwa mapenzi.

Lakini kama hiyo haitoshi, Nandy amemu-unfollow Billnas lakini pia Nenga na yeye amemu-unfollow Nandy kwenye mitandao ya Instagram.

Sekeseke hili linakuja ikiwa ni miezi 6 sasa tangu Billnas amvishe pete ya uchumba Nandy. Pete ambayo baadaye familia ya Nandy ilisema haiitambui kwa sababu haikufata utaratibu — Billnass alimvisha Nandy pete hiyo akiwa jukwaani.

Je, hiki kinachoendelea ni dalili ya kwamba penzi la wawili hawa linaelekea kuvunjika tena kwa mara ya pili? Kwa sababu waliwahi kuwa kwenye mapenzi kabla lakini wakaachana.