Wenger awachenjia wakongwe kina Henry

Muktasari:

Mastaa wa zamani wa Arsenal; Ian Wright, Thierry Henry, Lee Dixon, Paul Merson na Martin Keown, wamekuwa wakiwashambulia kwa maneno makali wachezaji wa sasa wa timu hiyo wakiwashutumu kwa kucheza hovyo.

LONDON, ENGLAND. Arsene Wenger amevunja ukimya na kuamua kuwachenjia nyota wa Arsenal katika kikosi hicho akiwaambia hata wao hakuna aliyekuwa bora.

Mastaa wa zamani wa Arsenal; Ian Wright, Thierry Henry, Lee Dixon, Paul Merson na Martin Keown, wamekuwa wakiwashambulia kwa maneno makali wachezaji wa sasa wa timu hiyo wakiwashutumu kwa kucheza hovyo.

Wenger alisema: “Siku zote nimekuwa na tatizo la kuelewa kinachosemwa na hawa magwiji. Nilikuwa na wachezaji wote hao, nao walikuwa na udhaifu wao kama ilivyo kwa wengine.