Timu ya Ligi Kuu Uholanzi yatoa zawadi Bongo
Muktasari:
Eefke Hagen na Emma van de Velde ni walimu ambao wakati wanakuja nchini waliamua kupitia kwenye timu hiyo na kupewa zawadi hizo.
Arusha. Timu ya Heerenveen ya Ligi Kuu nchini Uholanzi maarufu kama Eredivisie imetoa zawadi ya jezi na viatu kwenye Kituo cha Future Star's kilichopo jijini hapa.
Eefke Hagen na Emma van de Velde ni walimu ambao wakati wanakuja nchini waliamua kupitia kwenye timu hiyo na kupewa zawadi hizo.
"Tuliwapa maelezo kidogo kuhusu Future Stars na ndiyo maana hawakuona tatizo kutupa zawadi hizo chache kuwaletea, zitawasaidia," alisema Emma.
Future ni kituo cha kulelea vipaji vya soka kilichopo chini ya kocha mkuu, Afred Itael ambaye anasaidiwa na makocha wengine.