Nyota Venezuela anyimwa kibali cha kazi England klabu yake ya Watford yashangaa
Muktasari:
Penaranda aliyeiwezesha Venezuela kucheza fainali ya Kombe la Dunia la vijana chini ya miaka 20, mwezi huu na kufungwa bao 1-0 na England amekuwa akicheza Hispania kwa mkopo kwenye klabu ya Malaga.
Watford, England. Chama cha Soka England (FA) kwa msimu wa pili kimeinyima kibali cha kazi klabu ya Watford kwa kinda wao, Adalberto Penaranda raia wa Venezuela.
Penaranda aliyeiwezesha Venezuela kucheza fainali ya Kombe la Dunia la vijana chini ya miaka 20, mwezi huu na kufungwa bao 1-0 na England amekuwa akicheza Hispania kwa mkopo kwenye klabu ya Malaga.
Kwenye mchezo wa fainali, alikosa penalti na kuiacha timu ya England chini ya miaka 20 ikishinda Kombe la Dunia.
Kijana huyo alijiunga na Watford mwaka 2016 ametolewa mara tatu kwa mkopo.
Kocha wa England, Paul Simpson aliishauri FA impe kibali cha kazi, lakini amekataliwa kwa madai ya kukosa sifa
Maombi hayo ya kibali kwa raia wa Venezuela yalikataliwa juzi licha ya kung'ara akiichezea nchi yake kwenye Kombe la Dunia la Vijana chini ya miaka 20 nchini Korea Kusini.
Klabu ya Watford imeeleza kusikitishwa na uamuzi huo wa FA kwa mchezaji wao, Adalberto Penaranda ambaye alitarajiwa kuanza kuonyesha makali yake akiwa Ligi Kuu, EPL.
Kocha Simpson alieleza kuwa Penaranda anao uwezo wa kucheza na kung'ara akiwa England.