Wagombea wawili waekewa pingamizi uchaguzi wa TFF

Muktasari:

Waliowekewa pingamizi ni Wales Kiria ambaye amewekewa pingamizi na John Kijumbe, Mussa Sima na amewekewa pingamizi na Hussen Mwamba.

Dar es Salaam. Wagombe wa nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa Shirikisho la Soka (TFF), wamefika asubuhi kwa ajili ya usaili huku wawili kati  73 wakiwekewa pingamizi.

Waliowekewa pingamizi ni Wales Kiria ambaye amewekewa pingamizi na John Kijumbe, Mussa Sima na amewekewa pingamizi na Hussen Mwamba.

Mwenyekiti wa Kamayi ya Uchaguzi, Revocatus Kuuli alisema kuwa kabla ya kuanza usaili saa 6 kamili mchana wataanza kwa kusikiliza pingamizi hizo na baada ya kutoa majibu wataanza usaili.

"Tunaanza kwanza kusikiliza hizi pingamizi na kuzitolea majibu na halafu saa 6, kamili mchana ndio usaili utaanza kutokana na majina ya wagombea waliowahi kufika na kuandika jina mapema kwenye karatasi ya waliofika hapa leo," alisema Kuuli.

Kuuli alisema pia kwa wale wagombea ambao hawapo siku ya leo siku bado hazijaisha zimebaki siku mbili kwahiyo hata kama watakuwa na mapingamizi nao watawasikiliza pia.