Tshishimbi apewa fedha na king’amuzi

Dar es Salaam. Kiungo wa Yanga, Papy Tshishimbi amekabidhiwa zawadi yake ya Sh 1milioni baada ya kuwa mchezaji bora wa Februari.

 na wadhamini wadhamini wa ligi kuu Vpl baada ya kuibuka mchezaji bora wa mwezi Februari.

Tshishimbi amekabidhiwa zawadi hiyo na wadhamini wa Ligi Kuu baada ya awali kushindwa kuchukua tuzo hiyo kutokana klabu yake kuwa katika mashindano ya kimataifa.

Kiungo huyo alikabiziwa hundi ya shilingi milioni moja kutoka katika kampuni ya Vodacom pamoja na king’amuzi cha Azam Tv.

Katika tuzo hiyo Tshishimbi aliwabwaga Pius Buswita pamoja na Emmanuel Okwi, baada ya mwezi huo kufunga mabao matatu kwa Yanga na kutoa pasi moja ya mwisho iliyozaa bao.

Huku Buswita akiifungia mabao mawili kwa Yanga, Okwi aliisaidia Simba kupata pointi 10 katika michezo minne, baada ya kushinda mitatu na kutoka sare mchezo mmoja, pamoja na kuifungia timu yake mabao manne.

Katika mwezi huo pia, Buswita na Tshishimbi hawakupata kadi yoyote, lakini Okwi alipata kadi moja ya njano.