Tottenham yatangaza kumuachia Federico Fazio klabu ya Roma

Muktasari:

Hivyo klabu hizo mbili zimefikia mwafaka na Fazio atakuwa mchezaji wa kudumu wa Roma kuanzia msimu huu.

London, England. Klabu ya Tottenham imethibitisha kuachana na beki wake, Federico Fazio (39), ambaye alitolewa kwa mkopo msimu wote ulioisha kwa timu ya Roma.

Hivyo klabu hizo mbili zimefikia mwafaka na Fazio atakuwa mchezaji wa kudumu wa Roma kuanzia msimu huu.

Klabu hiyo ya Seria A imekubali kulipa gahara ma Pauni 2.8 milioni ili kumtumia mchezaji huyo kwa misimu inayofuata.